Isaiah 17:1-3

Neno Dhidi Ya Dameski

1 aNeno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji
bali itakuwa lundo la magofu.

2 bMiji ya Aroeri itaachwa
na itaachiwa mifugo ambayo italala huko,
bila yeyote wa kuyaogopesha.

3 cMji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu,
nao uweza wa ufalme kutoka Dameski;
mabaki ya Aramu yatakuwa
kama utukufu wa Waisraeli,”
asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Copyright information for SwhKC